Matthew 24:15-21

15 a “Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu), 16basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. 17 bYeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba. 18Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. 19 cOle wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! 20 dOmbeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato. 21 eKwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe.
Copyright information for SwhNEN